Posts

Uteuzi wa Dr. W.P.Slaa kuwa Balozi: Rais Magufuli Anaendelea Kujieleza na Kujipambanua Kisiasa

Image
  Mwanzo mwanzoni nikiri kuwa nimefarijika sana kwa uteuzi wa Dr. Wilbrod Peter Slaa kuwa Balozi. Uteuzi huo umefanywa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe Magufuli. Nimefurahi kwakuwa Dr. Slaa, kwa weledi wake, usomi wake, kwa sifa zake uzoefu wake na ubobezi anastahili uteuzi huo au wowote kwa ajili ya kuitumikia nchi. Kwa uteuzi wa Dr. Slaa kuwa Balozi, Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM anaendelea kujieleza na kujipambanua. Anajipambanua kuwa anasimamia kauli zake. Mara kwa mara hutamka kuwa 'maendeleo hayana chama'. Na akawahi kukaririwa akisema kuwa anaweza kumteua hata asiye mwanaCCM kama tu ana sifa. Akafanya hivyo kwa Mama Mghwira na kwa Prof. Kitila Mkumbo. Teuzi zake nje ya CCM, pamoja na kwamba zinaweza kuzua malalamiko, manung'uniko na maumivu kwa wanaCCM, zinajieleza na kujipambanua kuwa uwezo, uzalendo na uchapakazi ndiyo vigezo pekee vilivyobaki katika teuzi za Rais Magufuli. Kwake yeye, hakuna tofauti kati ya mwanaCCM au mw...

Dr. Luis Shika Natoa Milioni 1.5$ Za Kimarekani Kila Mwaka Shinyanga Wilayani Kahama

Image
                        Dr. Luis Shika Natoa Milioni 1.5$ Za Kimarekani Kila Mwaka Shinyanga Wilayani Kahama VIDEO:

Mugabe Kuhudhuria Kuapishwa kwa Emmerson Mnangagwa

Image
  Robert Mugabe anatarajiwa kuhudhuria kuapishwa kwa rais mpya wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa kulingana na runinga ya habari ya taifa hilo ZBC . Maandalizi yameanza katika uwanja wa kitaifa wa michezo katika mji mkuu wa Harare ambapo hafla hiyo itafanyika. Mwandishi wa maswala ya kidiplomasia Judith Makwanya amesema kuwa kiongozi anayeondoka anatarajiwa kukagua gwaride akitoa kwaheri huku kiongozi mpya akilijulisha jeshi katika sherehe hiyo ya gwaride. Tayari waziri wa Uingereza barani Afrika Rory Stewart amewasili nchini Zimbabwe mapema kulinga na chombo cha habari cha AFP. Mugabe: ''Naombewa nife'' Mugabe atakumbukwa kwa mabaya Rais Robert Mugabe amejiuzulu Afisa huyo amewasili tayari kuhudhuria kuapishwa kwa rais mpya siku ya Ijumaa. Bwana Sterwart anatarajiwa kukutana na viongozi wa kisiasa na wale wa kibiashara pamoja na makundi ya haki za kibinaadamu na mashirika yasiokuwa ya kiserikali kulingana na waziri wa maswala ya kigeni nchini Uingereza. Ametaja mabadiliko...

Emmerson Mnangagwa Kuapishwa Kumrithi Mugabe Kama Rais

Image
  Emmerson Mnangagwa anatarajiwa kuapishwa kama rais wa Zimbabwe, kufuatia kuondoka kwa rais kuondoka kwa Robert Mugabe madarakani baada ya miaka 37 ya utawala wa kiimla. Makamu huyo wa zamani wa rais ambaye alirejea kutoka uhamishoni Jumatano -ataapishwa kaka uwanja wa ndege wa Harare. Kufutwa kwake kazi mwezi huu kulipelekea chama tawala cha Zanu-PF na jeshi kuingilia kati na kumlazimisha Mugabe ang'atuke . Upinzani unamtaka Bwana Mnangagwa, ambae amekuwa mmoja wa watawala kumaliza "utamaduni wa ufisadi". Taarifa ya kuondoka madarakani kwa Mugabe mwenye umri wa miaka 93 hapo siku ya Jumanne iliibua sherehe kubwa kote nchini Zimbabwe Ilitolewa kwa njia ya barua bungeni na kikao cha kumpigia kura ya kutokuwa na imani nae kikakatizwa. Katika barua hiyo Bwana Mugabe alisema anajiuzulu ili kuruhusu mchakato rahisi na wa amani wa ukabidhianaji mamlaka na kwamba uamuzi wake ulikuwa wa hiari. Robert Mugabe na mkewe Grace tarehe 8 Novemba 2017Haki miliki ya pichaREUTERS Image c...

Mama Kanumba Aumizwa na Kifungo cha Lulu Ajipanga Kumtembelea Gerezani

Image
  MAMA wa staa wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Frola Mtegoa amesema kuwa, kutokana na matatizo yaliyompata staa wa filamu Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili, amekuwa akimuonea huruma na anajipanga kumtembelea gerezani. Akipiga stori na Ijumaa, Mtegoa alisema watu wengi wamekuwa wakihisi kuwa ana chuki na Lulu, lakini moyo wake unampenda na kama isingekuwa sheria kuhitaji Lulu kufungwa basi yeye asingekuwa na tatizo naye. Staa wa filamu Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ “Sina chuki na Lulu, tulikuwa karibu lakini nafikiri watu wake wanaozunguka ndiyo waliosababisha ukaribu wetu kuparanganyika. “Lakini moyoni ninampenda na kiimani mimi ni Mkristo. Kwa hiyo siwezi kufurahi kuona mwenzangu anapata matatizo, ipo siku nitamtembelea gerezani!” alisema mama huyo. 

Wolper Alia na Mastaa Kutomsapoti Katika Biashara Yake

Image
  STAA wa Bongo Movies, Jacquline Wolper amesema kuwa mastaa wengi hawapendi kupeana ‘sapoti’, kiasi kwamba hata kama staa mwenzao akiwa na biashara yake wapo radhi kununua kwingine lakini si kwake, ili tu wamkomoe. Akichonga na gazeti hili, Wolper alijitolea mfano kwa kusema kuwa tangu amejiingiza kwenye biashara ya ushonaji, watu wengi ambao wamekuwa wateja wa biashara zake ni wa kawaida tu na wasanii wenzike hawazidi hata watatu. “Unapofanya maendeleo kwa sisi mastaa wenzako si kwamba wanapenda.  Wananuna ndiyo maana huwezi kuwaona wakikusapoti,” alisema Wolper. 

Tanzia: Mbunge wa Songea Mjini Gama Kuzikwa Kijijini Kwao Likuyufusi

Image
  Aliyekua mbunge wa Songea Mjini (CCM), Leonidas Gama anatarajiwa kuzikwa Jumatatu katika makaburi ya familia yaliyopo Kijiji cha Likuyufusi mkoani Ruvuma. Gama aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo Ijumaa Novemba 24,2017 atazikwa Jumatatu Novemba 27,2017 katika makaburi hayo yaliyopo umbali wa kilomita 25 kutoka Songea mjini. Akizungumza na Mwananchi Issa Fussi ambaye ni msemaji wa familia na mdogo wa Gama amesema amefariki usiku wa kuamkia leo akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Misheni ya Peramiho. Amesema Gama alikuwa akisumbuliwa na shinikizo la damu na alipelekwa hospitalini hapo Jumatano Novemba 22,2017 usiku na kulazwa hospitalini hapo . Fussi amesema msiba huo ni pigo kwa familia kwa kuwa Gama alikuwa nguzo akitegemewa katika masuala mbalimbali ya maendeleo na kifamilia. Amesema mwili wa marehemu Gama umehifadhiwa katika Hospitali ya Peramiho na utaratibu wa mazishi unaendelea.